Sinopsis
Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.
Episodios
-
Rais Kagame na Makubaliano ya Washington DC na mazishi ya Albert Ojwang Kenya
05/07/2025 Duración: 20minYaliyoangaziwa katika makala hii ni pamoja na kauli ya rais wa Kenya kujenga kanisa ndani ya ikulu ya Nairobi, rais Paul Kagame wa Rwanda na mkataba wa amani ulioisainiwa kati ya nchi yake na DRC, waziri mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa kutogombea tena ubunge kuwakilisha jimbo la Ruangwa, hali nchini DRC, Sudan na kauli ya Ufaransa kuwa inatarajia Algeria kumsamehe mwandishi wa vitabu Boualem Sansal aliyefungwa, lakini pia mkutano wa viongozi wa Ulaya kule London Uingereza kufanyika wiki ijayo
-
Maandamano mapya yaua 16 Kenya, DRC na Rwanda zasaini makubaliano ya amani
28/06/2025 Duración: 20minWiki hii ulimwengu umeshuhudia matukio mengi ya ajabu na hatari sana kwa usalama wa nchi mbali mbali, kwanza nchini Kenya watu 16 waliuawa katika maandamano ya kuadhimisha mwaka mmoja wa mauaji ya vijana Gen Z, Rwanda na DRC zatia saini mkataba wa amani kumaliza vita vya mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, siasa za Chad, Zambia na pia mashambulizi kati ya Israeli na Iran, pamoja na mkutano wa jumuia ya NATO..na mengine mengi
-
Israeli na Iran zaendelea kushambuliana, matukio mengine duniani
21/06/2025 Duración: 20minMashambulio makubwa kwa makombora kati ya Israeli na Iran, na hali inayoendelea hadi sasa, maandamano ya kupinga kifo cha mwanablogu Albert Ojwang yaliyofanyika baada ya naibu Inspekta mkuu wa polisi Eliud Lagat kutangaza kujiuzulu nafasi kupisha uchunguzi, hali ya kisiasa nchini DRCbaada ya waziri wa sheria Constant Mutamba kujiuzulu, na vile vile siasa za ukanda wa Afrika mashariki, Afrika ya magharibi na kaskazini na kwengineko duniani.-
-
Mauaji ya mwanablogu nchini Kenya, Marekani yataka Jeshi la Rwanda kuondoka DRC
14/06/2025 Duración: 20minMengi yamejiri nchini Kenya na maeneo mengine wiki hii lakini kubwa ni maandamano ya kupinga mauaji ya kijana Albert Ojwang na kutaka maafisa wa polisi waliohusika wajiuzulu, wiki hii Marekani iliitaka nchi jirani ya Rwanda kuwaondoa wanajeshi wake kwenye ardhi ya DRC kabla ya kusainiwa kwa mkataba wa Washington, pia utasikiliza mengine mengi kwengineko duniani