Wimbi La Siasa

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 4:03:55
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa

Episodios

  • Uganda: Serikali yawasilisha mswada bungeni, kutaka raia kushtakiwa kwenye Mahakama za kijeshi

    14/05/2025 Duración: 10min

    Mswada tata, utakaoruhusu raia wa kawaida kushatakiwa kwenye Mahakama za kijeshi, umewasilishwa bungeni nchini Uganda, Mei 13, 2025. Upinzani unasema, lengo la mswada huo ni kuwalenga wanaopinga kiongozi wa muda mrefu Yoweri Museveni kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwaka 2026. Kwanini serikali ya Uganda inataka raia wa kawaida washtakiwe kwenye Mahakama za kijeshi ?

  • Rwanda na DRC zawasilisha mapendekezo kuhusu mkataba wa amani

    07/05/2025 Duración: 10min

    Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, zimewasilisha mapendekezo ya rasimu ya mkataba wa amani kwa Marekani, kujaribu kutafuta mzozo wa Mashariki mwa DRC. Nchi hizo mbili zinatarajiwa kutia saini mkataba wa kudumu mwezi Juni, jijini Washington. Harakati hizi, zitazaa matunda ?

  • Kenya: Upinzani utamtikisa Ruto uchaguzi wa mwaka 2027 ?

    30/04/2025 Duración: 10min

    Wanasiasa wakuu wa upinzani nchini Kenya, wakiongozwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua, Aprili 29 2025, walikutana jijini Nairobi kuanza mikakati ya kuunda muungano mpya, kwa maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Je, muungano huu ambao pia umemjumuisha aliyekuwa Waziri wa usalama Fred Matiang’i, unaweza kumtikisa rais William Ruto  wakati wa uchaguzi huo ?

  • DRC: Kabila aripotiwa kufikia Goma, huku chama chake kikifungiwa

    23/04/2025 Duración: 10min

    Rais wa zamani wa DRC, Joseph Kabila, Aprili 18, aliripotiwa kurejea nchini na kufikia jijini Goma, linalodhibitiwa na waasi wa M 23. Hata hivyo, taarifa hizi hazijathibitishwa rasmi. Serikali jijini Kinshasa, nayo imesitisha shughuli zote za kisiasa za chama chake cha PPRD. Kabila anashtumiwa na serikali kwa kuunga vitendo vya waasi hao.

página 2 de 2