Jukwaa La Michezo

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 9:28:59
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala haya yanaangazia maendeleo ya michezo mbalimbali Ulimwenguni na pia huwa haiwaweki kando wanamichezo waliobobea na vilevile kufanya uchanganuzi wa kina wa michezo wakati wa mashindano mbalimbali. 

Episodios

  • CAF: Simba kuchuana na RS Berkane leo kwenye fainali ya Kombe la Shirikisho

    17/05/2025 Duración: 23min

    Leo tumekuandalia mengi ikiwemo fainali ya kombe la shirikisho la CAF kati ya Simba na RS Berkane, fainali za Afcon U20, Congo Brazaville yarejeshwa katika soka ya kimataifa, droo kamili ya michuano ya Chan 2024, mkondo wa Nile katika ligi ya basketboli ya Afrika, tuzo za wanasoka bora ligi kuu ya Uingereza.

  • BAL: APR ya Rwanda inalenga fainali za Afrika watakaposhiriki mara ya pili

    10/05/2025 Duración: 23min

    Leo tumeangazia michuano ya Afcon U20 ambayo imeingia hatua ya mtoano, ripoti maalum kuhusu APR inapojiandaa kushiriki BAL kwa mara ya pili, debi za soka nchini Kenya na Tanzania zayumbayumba, promota wa ndondi kutoka Uganda ahamia nchini Kenya, uchambuzi wa fainali za ligi za klabu bingwa Ulaya, mechi ya kwanza ya Evra kwenye ndondi ya kuchanganywa yaahirishwa huko Paris huku Mohammed Salah akishinda tuzo lake la tatu la waandishi wa habari za soka

  • AFCON U20: Michuano ya vijana ya soka yang'oa nanga nchini Misri

    03/05/2025 Duración: 23min

    Hii leo tumeangazia michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya vijana chini ya miaka 20 kuanza nchini Misri, mkondo wa mtoano katika msururu wa raga duniani, diamond league mkondo wa pili huko Uchina na Ligi ya Basketboli mkondo wa Sahara ukiendelea, Cecafa yapata rais mpya, nembo ya Visit Rwanda yaendelea kupanuka, bondia wa DRC Martin Bakole kupigana leo usiku, PSG, Man Utd, Spurs na Chelsea zavuna matokeo mazuri kwenye nusu fainali ligi za vilabu bingwa ulaya.

  • Riadha: Ni nani atashinda mbio za London Marathon mwaka 2025?

    26/04/2025 Duración: 24min

    Leo tumeangazia michuano ya klabu bingwa kufuzu fainali, riadha za Diamond League, Boston na London Marathon, Cameroon yafuzu Kombe la Dunia la U17, uchaguzi wa kamati ya Olimpiki nchini Kenya watibuka, Gor Mahia yanuia kujenga uwanja wao, uchambuzi wa debi ya El Clasico huku Carlos Alcaraz akijiondoa kwenye mashindano ya Madrid Open.

página 2 de 2