Sinopsis
Makala haya yanaangazia maendeleo ya michezo mbalimbali Ulimwenguni na pia huwa haiwaweki kando wanamichezo waliobobea na vilevile kufanya uchanganuzi wa kina wa michezo wakati wa mashindano mbalimbali.
Episodios
-
CAF: Simba yatinga nusu fainali michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika
12/04/2025 Duración: 24minTuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa matokeo ya robo fainali mechi za klabu bingwa Afrika, Uganda yalenda kufuzu Kombe la Dunia wasiozidi miaka 17, timu ya taifa ya raga ya kina dada ya Kenya yalenga kurejea katika msururu wa dunia, michuano ya vilabu ya Afrika mchezo wa voliboli, Rwanda yaadhimisha miaka 31 michezoni tangu mauaji ya kimbari, Maluki atangaza nia ya kuwania urais wa Nock, Salah asaini kandarasi mpya Liverpool, Real Madrid itageuza meza dhidi ya Arsenal?
-
Raga: Nafasi ya Shujaa 7s kusalia kwenye msururu wa raga duniani ni gani?
05/04/2025 Duración: 23minLeo kwenye kipindi tumeangazia mkondo wa kwanza robo fainali ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika, matokeo ya Uganda na Tanzania kwenye michuano ya AFCON U17 huk Morocco, nafasi ya Shujaa 7s ya Kenya kusalia kwenye msururu wa raga duniani, mnyarwanda Celestine Nsanzuwera ashinda michuano ya gofu ya Sunshine Tour Afrika Mashariki, wachezaji watano wa ufaransa wa tenisi wapokea adhabu kwa makosa ya upangaji matokeo, Muller na De Bruyne kuondoka vilabuni mwao mwishoni mwa msimu huu.
-
Kenya: Nani atatamba kwenye "Debi ya Mashemeji" AFC Leopards vs Gor Mahia?
29/03/2025 Duración: 23minMiongoni tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo ya raga mkondo wa HongKong 7s, sakata la upangaji mchezaji dhidi ya golikipa wa Kenya Patrick Matasi, maandalizi ya debi ya Mashemeji, Misri yapewa haki za kuandaa AFCON U20 huku CAF ikiifungulia uwanja wa Benjamin Mkapa, tuzo nono kwa washindi wa Kombe la Dunia la vilabu, kocha wa Brazil atimuliwa naye Djokovic akikaribia kushinda taji lake la 100.
-
Mashindano ya kukimbiza magari, yapamba moto nchini Kenya
22/03/2025 Duración: 23minMashindano ya dunia ya kukimbiza magari, Safari Rally yanaendelea nchini Kenya. Madereva mbalimbali kutoka duniani, wanakutana mjini Naivasha kwa ajili ya kutafuta ubingwa wa mwaka 2025.