Jua Haki Zako

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 3:58:22
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.

Episodios

  • Kenya : Vijana wazidi kuandamana

    01/07/2025 Duración: 09min

    Kwa wiki za hivi karibuni zimekuwa za misukosuko nchini Kenya, mitaa ya jiji la Nairobi na miji mingine mikuu imekuwa ikifurika vijana… wakiwa na mabango mikononi, miili yao ikiwa tayari kwa chochote — hata kwa  gesi ya kutoa machozi  na risasi. Lakini maandamano haya yanamaanisha nini? Vijana hawa wanadai nini? Na wanaruhusiwa kisheria kufanya hivyo? Ndio maswali tutakayokuwa tunayajibu kwenye makala haya.   Karibu katika makala ya Jua Haki Zako – makala ambayo siku zote hukuelemisha kuhusu haki zako tena za msingi jina langu ni benson Wakoli

  • EAC : Haki za wanawake maeneo ya vita

    24/06/2025 Duración: 09min

    Katika kila kona ya dunia, sauti za wanawake zimekuwa zikipigania jambo moja kuu – haki. Haki ya kusikilizwa,  Haki ya kuthaminiwa, Haki ya kupewa nafasi sawa. Na hapa Africa Mashariki  ingawa hatua zimepigwa, safari ya mwanamke kuelekea usawa bado ina changamoto, katika hali ya vita kama vile, Mashariki mwa DRC, nchini Sudan Kusini na kaskazini, kaskazini mwa Ethiopia na pia Musumbiji. Skiza makala haya kufahamu juhudi zinafanywa na shirika la Women For Women kutetea haki za wanawake kwenye maeneo ya vita, licha misaada kupunguzwa.

  • DRC : Haki ya wanawake Mashariki mwa DRC

    23/06/2025 Duración: 10min

    Katika makala haya  tunajikita kuangazia hali ya haki ya wanawake Mashariki mwa DRC baada waasi wa M23 kufaulu kudhibiti miji ya Goma na Bukavu. Tunazungumza na wakili Maggie Mkulima Shukru kutoka jijini Bukavu kutueleza hali ilivyo mashariki mwa DRC. Skiza makala haya kufahamu mengi.

  • Kenya: Haki ya matumizi ya vyombo vya dijitali

    10/06/2025 Duración: 10min

    Kadri Afrika inavyozidi kuingia katika ulimwengu wa  kidijitali, kila siku mamilioni ya watu wanaingia mitandaoni—kutafuta taarifa, kuwasiliana, kufanya biashara na hata kushiriki mijadala ya kisiasa. Lakini swali kuu ni Je, watu wote wanaelewa haki zao katika mazingira haya mapya ya kidijitali? Skiza makala haya kufahamu mengi.

página 2 de 2