Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 8:02:03
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.

Episodios

  • Wanafunzi zaidi ya 200 watekwa Nigeria, tume ya kuchunguza vurugu Tanzania yaapishwa

    22/11/2025 Duración: 19min

    Habari kuu wiki hii ni siasa za Tanzania zilizosababisha kuundwa kwa tume ya kuchunguza mauaji ya baada ya uchaguzi, kule DRC athari ya mafuriko, tutaangazia ripoti ya WHO kuhusu dhulma dhidi ya wanawake, kule Nigeria tutaangalia utekaji nyara wa wanafunzi zaidi ya 200 pia Mkutano wa G20 kufanyika wikendi hii Afrika Kusini Marekani ikisusia. Mkutano wa COP30 wakamilika Brazil bila mwafaka kuhusu kuachana na mafuta kisukuku. 

  • Rais Samia atoa msamaha kwa vijana waliokamatwa kwenye maandamano

    15/11/2025 Duración: 20min

    Miongoni mwa tarifa utakazoskia katika makala haya ni pamoja na, Rais wa Tanzania Samia Suluhu, ameagiza vyombo vya sheria kuangalia uwezekano wa kuwafutia mashtaka ya uhaini mamia ya vijana waliokamatwa kufuatia vurugu za uchaguzi wa Octoba 29, lakini hayo yakijiri kesi ya uhaini inayomkabili kiongozi wa CHADEMA Tundu Lissu ilihairishwa kwa muda usiojulikana.

  • Uchaguzi mkuu Tanzania: Waangalizi wasema haukuzingatia vigezo vya demokrasia

    11/11/2025 Duración: 20min

    Katika makala yetu leo tunaangazia pakubwa Uchaguzi Mkuu nchini Tanzania ambapo Rais Samia Suluhu aliapishwa siku ya Jumatatu kuongoza muhula wa pili, hata hivyo ni uchaguzi ambao ulikumbwa na utata huku waangalizi kutoka jumuiya ya Afrika kusini SADC na wale wa umoja wa Afrika AU wakisema haukuzingatia vigezo vya demokrasia. Tunaangazia pia taarifa ya Rais Paul Biya, wa Cameroon kuapishwa Alhamisi iliyopita kuongoza nchi hiyo kwa muhula wa nane, huku upinzani ukiitisha maandamano kupinga matokeo yaliyompa Biya ushindi. Lakini pia tutaangazia kongamano la kimataifa la mazingira, COP30 ambalo linafanyika huko Belem, nchini Brazil, kati ya Novemba 10 na 21.

  • Vurugu zaugubika Uchaguzi mkuu nchini Tanzania na hali nchini DRC

    04/11/2025 Duración: 20min

    Uchaguzi mkuu uliofanyika katika Jamhuri ya muungano wa Tanzania, na ambao uligubikwa na maandamano; mkutano wa Paris nchini Ufaransa kuhusu amani ya mashariki mwa DRC na eneo la maziwa makuu, siasa za nchini Kenya, Uganda lakini pia mauaji yaliyotekelezwa na kundi la RSF nchini Sudan, hali nchini Cameroon na Madagascar, kurejewa kwa mashambulizi nchini Ukraine, na huko Israeli dhidi ya Hamas

  • Rais W.Ruto amtunuku hayati Raila Odinga, nishani ya juu zaidi, hali mashariki ya DRC

    25/10/2025 Duración: 20min

    Hatua ya rais wa Kenya William Ruto kumtunuku aliyewahi kuwa waziri Mkuu na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, hayati Raila Odinga, nishani ya juu zaidi nchini, kukamatwa kwa makamu mwenyekiti wa chama cha Chadema nchini Tanzania, John Heche, DRC na Rwanda zakubaliana juu ya mchakato wa upatikanaji wa amani chini ya upatanisho wa Marekani, uchaguzi wa urais nchini Cote D’Ivoire, na rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarcozy wiki hii alianza kukitumikia kifungo cha miaka mitano.

  • Kenya yaomboleza kifo cha RAILA, Jukwaa jipya la kisiasa DRC lazinduliwa

    18/10/2025 Duración: 20min

    Miongoni mwa matukio makubwa yaliyojiri wiki hii ni pamoja na wakenya kuomboleza kifo cha mwanasiasa mashuhuri aliyewahi kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo Raila Amolo Odinga, kuzinduliwa kwa jukwaa jipya la kisiasa : Okoa DR Congo, kuendelea kwa kampeni za kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu kule Tanzania, kuapishwa kwa kiongozi wa kijeshi wa Madagascar, na matukio mengine duniani.

  • Jeshi la Israeli kuondoka Gaza, rais wa DRC aitaka Rwanda kuchangia amani

    11/10/2025 Duración: 20min

    Habari kuu wiki hii ni pamoja Israel kuanza kuwaondoa wanajeshi wake kwenye baadhi ya maeneo ya  Gaza, rais wa Ufaransa amteua tena Sebastien Lecornu kuwa waziri mkuu huku kukiwa na mvutano wa kisiasa, rais wa DRC, Félix Tshisekedi, amtaka mwenzake wa Rwanda, Paul Kagame, kuwaamuru waasi wa M23 kuacha vita mashariki mwa Congo, siasa za kikanda, yaliyojiri huko Morocco, mwanaharakati wa demokrasia nchini Venezuela, Maria Corina Machado, ndiye mshindi wa tuzo ya amani ya Nobeli ya mwaka wa 2025

  • Hukumu ya kifo dhidi ya rais mstaafu wa DRC, kampeni za uchaguzi nchini Uganda

    04/10/2025 Duración: 20min

    Kumekuwa na hisia mseto kuhusu hukumu ya kifo iliyotolewa dhidi ya rais mstaafu wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, Joseph Kabila, uzinduzi wa kampeni kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani nchini Uganda, hali ya nchini Tanzania wakati huu wananchi wakijiandaa kushiriki uchaguzi wa oktoba 29 mwaka huu, maandamano ya vijana Gen Z nchini Madagascar, na mashambulio ya mjini Manchester Uingereza.Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kusikiliza zaidi 

  • Mkutano wa 80 wa Umoja wa mataifa, hali ya DRC na maandalizi ya uchaguzi Uganda

    27/09/2025 Duración: 20min

    Baadhi ya habari ambazo tumezipa uzito ni pamoja na mkutano wa 80 wa baraza kuu la umoja wa mataifa wiki hii ambapo viongozi wa dunia walipata nafasi ya kutoa hotuba zao, kujiuzulu kwa spika wa bunge la DRC Vital Kamerhe, na kuendelea kwa mapigano mashariki mwa nchi hiyo, kuidhinishwa kwa wagombea wa kiti cha urais nchini Uganda kuelekea uchaguzi wa mwakani, Peter Mutharika kurejea madarakani baada kupata ushindi kwenye uchaguzi mkuu, kura ya maoni ya Guinea, na mambo mengine mengi.

  • Kesi ya rais mstaafu wa DRC kurejelewa, mbio za baiskeli kung'oa nanga huko Rwanda

    20/09/2025 Duración: 20min

    Baadhi ya habari ambazo tumezipa uzito ni pamoja na vurugu katika bunge la DRC na mchakato wa kumuondoa spika wa bunge hilo na maafisa wengine, mashindano ya dunia ya baiskeli kung’oa nanga siku ya Jumapili mjini Kigali, mji mkuu wa Rwanda, siasa za Uganda kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani, tumeangazia hali nchini Tanzania, Sudan kusini, uchaguzi wa Malawi, kura ya maoni kule Guinea kuhusu marekebisho ya katiba na ziara wa Marekani huko Uingereza.

  • Zaidi ya watu 80 wafariki katika ajali ya boti Basankusu

    13/09/2025 Duración: 19min

    Karibu kwa makala ya Yaliyojiri wiki hii. Baadhi ya habari ambazo tumezipa uzito wiki hii ni makamu wa kwanza wa rais wa Sudan Kusini ashatkiwa kwa uhaini na mauaji, ajali ya boti nchini DRC. Tutaangalia hatma ya mkutano wa hali ya hewa nchini Ethiopia, Vilevile onyo la vifo vya malaria kuongezeka mwaka huu kutokana na kupunguzwa kwa misaada ya kigeni.

  • Hukumu dhidi ya waziri Mutamba nchini DRC, athari za misaada ya kigeni watoto wakizaliwa na HIV

    10/09/2025 Duración: 20min

    Wiki hii taarifa zilizokuwa gumzo kwenye vyombo vya habari ni kuhusu hukumu dhidi ya aliyekuwa waziri wa sheria nchini DRC, Constant Mutamba, nitakujuza pia kuhusu kampeni za uchaguzi mkuu nchini Tanzania, tutaangalia pia ajali ya boti nchini Nigeria iliyoua watu 30. Kimataifa, tutaangazia punde zaidi katika mzozo wa Urusi na Ukraine.

  • Kampeni za uchaguzi wa Tanzania, mapigano DRC, Urusi yaendelea kuishambulia Ukraine

    30/08/2025 Duración: 20min

    Kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu wa urais wa mwezi oktoba mwaka huu nchini Tanzania, kauli ya rais wa Rwanda Paul Kagame dhidi ya mzozo wa mashariki mwa DRC, mapigano makali kati ya jeshi la Congo FARDC na washirika wao wazalendo maeneo ya milima ya Fizi, hali nchini Sudan, ziara ya rais wa senegal jijini Paris ufaransa, Urusi yaendeleza mashambulio huko Kiev Ukraine licha ya shinikizo za Kimataifa na mengineyo.

  • Mkutano wa Trump na rais wa Ukraine na wakuu wa Ulaya, hali ya mashariki mwa DRC

    30/08/2025 Duración: 20min

    Ni juma ambalo limeshuhudia mkutano kati ya rais wa Marekani Donald Trmp na rais wa Ukraine Volodmir Zelensky akisindikizwa na viongozi wa Ulaya, michuano ya CHAN kwenye nchi tatu za Afrika Mashariki yaendelea, mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu juma hili yalishutumu jeshi la Rwanda likishirikiana na waasi wa M23 kuwaua raia wa kawaida Binza wilayani Rutshuru mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, mkutano wa kimataifa wa Tokyo kuhusu maendeleo ya Afrika au TICAD ulifunguliwa jijini Yokohama, Japani.

  • Mkutano wa uswis watamatika bila mkataba wowote, mapigano Ituri DRC yaua 31

    16/08/2025 Duración: 20min

    Mkutano wa Geneva washindwa kupata mkataba wa kimataifa kuhusu taka za plastiki,  takriban watu 31 wakiwemo raia 19 waliuawa katika mapigano kati ya jeshi la Kongo na wanamgambo wa CRP wa Thomas Lubanga katika eneo la Djugu mkoani Ituri kaskazini mashariki mwa DRC, michuano ya CHAN 2024 kwenye nchi za Afrika Mashariki, hali ya Sudan, Somalia na mkutano wa rais wa Marekani Donald Trump na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin, huko Alaska.

  • Sintofahamu yaendelea kuhusu kuanza kwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Kinshasa na M23

    09/08/2025 Duración: 20min

    Miongoni mwa taarifa utakazoziskia ni pamoja na; sintofahamu yaendelea kuhusu kuanza kwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Kinshasa na Muungano wa Vikosi vya Kidemokrasia vya Ukombozi wa Kongo AFC/M23, Rais wa DRC, Felix Tshisekedi amefanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri na kujumuisha upinzani. Tutakueleza punde zaidi katika uchaguzi wa Tanzania. Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Afrika Magharibi na eneo la Sahel, yasema hali ya usalama katika eneo hilo inasalia kuwa ya wasiwasi mkubwa na kimataifa Rais wa Marekani, Donald Trump, asema huenda hivi karibuni akakutana ana kwa ana na rais wa Urusi, Vladmir Putin, kuzungumzia mzozo wa Ukraine.

  • Jumuiya za EAC na SADC kuujadili mzozo wa mashariki mwa DRC, hali ya Gaza

    02/08/2025 Duración: 20min

    Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo juma hili zilifanya mkutano wa kwanza wa kamati ya pamoja ya usimamizi , kesi ya rais wa zamani wa DRC Joseph Kabila ilisikilizwa kwa mara ya pili mjini Kinshasa, serikali ya Tanzania, ilipiga marufuku raia wa kigeni kufanya biashara ndogondogo, hali nchini Sudan kusini na Sudan, hatua ya rais wa Cote D’Ivoire kutangaza nia ya kuwania urais kwa muhula wa nne na kwengineko duniani.

  • Kesi ya rais mstaafu wa DRC J.Kabila yasikilizwa, mapigano kati ya Thailand na Kambodia

    26/07/2025 Duración: 20min

    Kesi ya rais wa zamani wa DRC Joseph Kabila ilifunguliwa mjini Kinshasa, waziri wa zamani wa sheria nchini DRC Constant Mutamba alikana mashtaka dhidi yake Kuhusu ubadhirifu wa fedha za umma, ripoti moja wiki hii ilisema Watu 65 waliuawa nchini Kenya kufuatia maandamano ya vurugu kati ya mwezi juni na julai, hali nchini Sudan kusini na Sudan lakini pia tutaangazia Afrika magharibi na mengine mengi

  • DRC na waasi wa M23 kukubaliana kuhusu amani ya mashariki, Humphrey polepole akosoa CCM

    19/07/2025 Duración: 20min

    Serikali ya Kinshasa na waasi wa AFC/M23 mbioni kusaini makubaliano ambayo kimsingi yanaleta matumaini ya kufikia amani mashariki mwa nchi hiyo, Tanzania yazindua dira ya maendeleo 2050 kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba, umoja wa mataifa wasema hali ya kibinadamu nchini Sudan si ya kuridhisha, rais Paul Biya, kiongozi mkongwe sana duniani na umri wa miaka 92 kuwania urais kwa muhula wa nane, umoja wa ulaya kutishia kuiwekea Urusi vikwazo vipya na hali ya nchini Syria

  • Rais Ruto aibua hisia kali kwa kuwaagiza polisi kuwapiga risasi ya miguu waandamanaji

    12/07/2025 Duración: 20min

    Wiki hii watu wasiopungua 38 waliuawa nchini Kenya kufuatia maandamano ya SabasAba siku ya Jumatatu. Rais Ruto aliibua hisia kali alipowaagiza polisi kuwapiga risasi ya miguu waandamanaji. Lakini pia, malalamiko yaliwasilishwa rasmi huko Brussels, dhidi ya wanafamilia tisa wa rais wa DRC Félix Tshisekedi, ambao wana uraia wa Ubelgiji, wakituhumiwa kwa wizi wa madini ya nchi yao. Tutakujuza pia taarifa za kikao cha Rais wa Marekani Donald Trump na marais sita wa Afrika magharibi kilichofanyika, lakini pia Uingereza na Ufaransa kutangaza rasmi mpango wa majaribio wa kuwarudisha Paris baadhi ya wahamiaji wanaowasili nchini humo kwa kutumia boti ndogo.

página 1 de 2