Habari Rfi-ki

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 3:56:53
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

Episodios

  • Kikao cha usalama wa DRC na Sudan chakamilika Ethiopia bila suluhu

    17/02/2025 Duración: 10min

    Makala ya leo yanaangazia Kikao cha viongozi wa Afrika, kilichotamatika rasmi mwishoni mwa juma lililopita nchini Ethiopia, mzozo wa DRC na Sudan ukigubika mijadala yao.Hata hivyo vikao hivyo  vimekamilika  bila suluhu ya mizozo ya nchi zote mbili, ambapo vyongozi  waliishia kwa kutoa wito wa kusitisha mapigano. tulimuuliza msikilizaji iwapo anaridhika na matokeo ya kikao hicho na  anadhani nini cha zaidi viongozi hawa wangefanya kukomesha mizozo barani Afrika

  • Mkutano wa kila mwaka wa Umoja wa Afrika kuzingatia usalama wa DRC

    13/02/2025 Duración: 10min

    Mkutano wa kila mwaka wa viongozi wa Afrika umeanza rasmi jijini Addis Ababa, #Ethiopia ambapo maswala muhimu ikiwemo usalama mashariki mwa #DRC, mapinduzi ya kijeshi na vita dhidi ya makundi ya kijihadi yakitarajiwa kugubika mkutano huu.Tulimuuliza mskilizaji natarajia nini kipya kutoka kwa viongozi wa AU? na iwapo anafikiri viongozi wameshindwa kumaliza changamoto za bara hili..

  • Kauli ya rais Donald Trump kuhamisha wapalestina yapingwa vikali

    12/02/2025 Duración: 10min

    Kwenye kipindi cha leo tunaangazia kauli  tata ya Rais Donald #trump, kuhusu mzozo wa #Gaza, safari hii akitishia kuvunjika kwa mkataba wa usitishaji mapigano, ikiwa Hamas haitawaachia mateka wote ifikapo Jumamosi ya wiki hii.Juma lililopita alidai kuwa nchi yake itachukua udhibiti wa Gaza na kuwahamisha Wapalestina.Tulimuuliza mskilizaji anazungumziaje kauli hiyo ya Trump and je huenda zikachochea mzozo zaidi kati ya #Israel na Hamas?

  • Hatua ya Kenya kuondoa mahojiano kwa waomba vitambulisho yaibua hisia mseto

    11/02/2025 Duración: 09min

    Makala haya yanaangazia hatua ya Serikali ya kenya  kusema  hakutakuwa na haja ya mahojiano kwa waomba vitambulisho toka katika maeneo ya mpakani, uamuzi ambao umeibua mjadala kuhusu masuala ya usalama.Tulimuuliza msikilizaji anazungumziaje hatua hiyo ya Kenya  vile vile nchini mwake hali ikoje

  • Kauli ya mkutano wa SADC na EAC kuhusu amani nchini DRC waibua maoni mseto

    10/02/2025 Duración: 09min

     kwenye makala ya leo tunaangazia  hatua ya  wakuu wa nchi za #SADC na EAC kutaka kusitishwa mapigano maramoja ,na kutaka  kuondoka kwa vikosi vya kigeni mashariki mwa #DRC, pamoja na Serikali ya Kinshasa kuzungumza moja kwa moja na waasi wa #M23 ambapo  wito huo  umepokelewa kwa hisia mseto na raia wa ukanda.

  • Kila siku ya Ijumaa huwa tunaangazia mada huru kwenye makala habari rafiki

    31/01/2025 Duración: 10min

    Kila siku ya  ijumaa ni mada huru  ambapo Tunampa nafasi  msikilizaji kujadili suala lolote ambalo limetokea nchini mwake wiki hii au kile ambacho amekisikiliza kwenye habari zetu juma hili.

  • Changamoto za upatikanaji wa Nishati ya Uhakika barani Afrika

    30/01/2025 Duración: 09min

    Wakuu wa nchi za Afrika walikutana juma hili nchini Tanzania ambapo walijadiliana kuhusu changamoto za upatikanaji wa Nishati ya Uhakika katika mataifa hayo.Licha ya rasilimali za bara la Afrika bado hakuna nishati ya uhakika na endelevu? Bonyeza uskilize maoni mbalimbali.

  • Athari za Donald Trump kusitisha misaada kwa Afrika na njia mbadala kujitegemea

    30/01/2025 Duración: 10min

    Uamuzi wa Rais wa Marekani #DonaldTrump, kuagiza kusitishwa kwa muda utowaji wa misaada yote ya kigeni umeibua mjadala na sintofahamu hasa kwa nchi za Afrika, ambazo sekta muhimu ikiwemo afya zinategemea msaada wa Marekani.Tulimuuliwa msikilizaji anazungumziaje hatua hii ya Marekani na Nchi za Afrika zifanye nini kuacha kutegemea misaada ya nchi za Kigeni?

  • Swali: Je viongozi wa Afrika wanaweza kutatua migogoro inayokumba bara hilo

    29/01/2025 Duración: 09min

    Mizozo inayosibu ukanda wa Afrika ya Mashariki inaendelea kuongezeka, ikiwemo Sudan Kusini na sasa DRC. Viongozi wa Afrika wanasisitiza matatizo ya Afrika sharti kutatuliwa kwa suluhu kutoka Afrika. Je hili linawezekana?

  • Wito wa mataifa ya Afrika kutafuta suluhu kwa matatizo ya Afrika

    29/01/2025 Duración: 06min

    Ukanda wa Afrika unazidi kushuhudia ongezeko la migogoro huku viongozi wakisisitiza Afrika ina majibu ya mizozo hiyo

  • Nani wa kulaumiwa kuhusu vita vinavyoendelea mashariki mwa DRC

    23/01/2025 Duración: 10min

    Mapigano kati ya waasi wa  M23 na wanajeshi wa serikali ya  DRC yanayoendelea na sasa yamefika jimboni Kivu Kusini,Tume ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia masuala ya kibinadamu OCHA ikisema maelfu ya watu wameendelea kukimbia makaazi yao.Kwenye makala haya tumemuuliza msikilizaji  nani wa kulaumiwa kuhusu vita hivi vinavyoendelea? na anafikiri ni kwanini imekuwa vigumu kupata suluhu?

  • Visa vya uchimbaji madini haramu vinazidi kuongezeka barani Afrika

    22/01/2025 Duración: 09min

    Visa vya uchimbaji wa madini haramu   vimeongezeka katika nchi mbalimbali barani Afrika .Afrika Kusini ikiwa  mfano wa nchi hizo ambayo imeshuhudia miili ya wachimba midogo zaidi ya 70 ikipatikana katika mgodi wa dhahabu usiokuwa rasmi.Kwenye kipindi cha leo tumemuuliza msikilizaji  anafkiri nchi za Afrika zimeshindwa kudhibiti uchimbaji haramu wa madini ? na nini kinaweza kufanyika kuzuia uchimbaji huo haramu ?

  • Dunia itarajie nini kutoka kwa uongozi wa Rais wa Marekani Donald Trump

    21/01/2025 Duración: 09min

    Kwenye kipindi cha leo tunaangazia kurejea afisini  kwa rais wa Marekani Donald Trump baada ya kuapishwa kama rais  na kuahidi nchi mpya.Tumemuuliza msikilizaji dunia itarajie nini  kutoka kwa uongozi Wake na je Waafrika wana matumaini gani kuhusu kuongozi wake Trumpµ?

  • Wataalamu wa afya kutoka jumuia ya EAC wakutana Mombasa pwani ya Kenya

    15/01/2025 Duración: 10min

    Makala ya habari rafiki imewashirikisha wasikilizaji kutoka kila kona ambapo wasikilizaji wametoa maoni yao kuhusu namna ambavyo wataalamu wa afya kutoka nchi za jumuia ya Afrika Mashariki walivyojadiliana kuhusu utaratibu wa kupata vibali kwenye nchi hizo bila ya kusumbuliwa. Ungana na Ruben Lukumbuka kusikiliza zaidi.

  • Kila siku ya Ijumaa kwenye makala Habari Rafiki ni Mada Huru

    03/01/2025 Duración: 10min

    Kila siku ya Ijumaa ni Mada huru  ambapo tunakupa nafasi msikilizaji kuchangia suala lolote ambalo limetokea nchini mwake au kile ambacho amekisikia katika matangazo yetu ya wiki hii.

  • Viongozi wa Afrika mashariki watoa wito wa amani kwenye hotuba ya mwaka mpya

    02/01/2025 Duración: 10min

    Katika salamu zao za mwaka mpya, viongozi karibu wote wa ukanda wa Afrika Mashariki, wametoa wito wa umoja na amani, huku kwa mataifa yenye utovu wa usalama, viongozi wakiahidi kirejesha utulivu.Tulimuuliza mskilizaji iwapo kiongozi wa nchi yake atabadili mambo mwaka huu wa 2025

  • Dunia yaukaribisha mwaka mpya wa 2025 huku viongozi wakiomba amani

    01/01/2025 Duración: 10min

    Mataifa mbalimbali duniani wakiwemo raia wa ukanda wa Afrika Mashariki, wamesherehekea mwaka mpya wa 2025 kwa kila aina ya mbwembwe na shamrashamra, kukiwa na hisia mseto za matumaini tofauti na mwaka uliopita.Tulimuuliza mskilizaji atueleze aliukaribisha mwaka mpya vipi na akiwa wapi,vile vile angependa kuona kipi kinabadilika kwenye nchi yake.

  • Matumizi ya mitandao ya kijamii nchini Kenya yaibua hisia mbalimbali

    31/12/2024 Duración: 10min

    Nchini Kenya mjadala mkali kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii unaendelea, ambapo baadhi wamekuwa wakiitumia kuikosoa Serikali na rais William Ruto, kwa kiwango ambacho wengine wanasema wakosoaji wamevuka mipaka huku baadhi wakisema watu wako huru kukosoa wanavyotaka.Tulimuuliwa mskilizaji je anaamini iwapo vijana wamevuka mipaka au la.

  • Umoja wa mataifa,waidhinisha kikosi kipya cha kulinda amani nchini Somalia

    30/12/2024 Duración: 10min

    Baraza la usalama la umoja wa Mataifa, mwishoni mwa juma limepitisha azimio kuunga mkono uundwaji wa kikosi kipya cha bara Afrika cha kulinda amani nchini Somalia, kikosi hiki kikichukua nafasi ya kile cha ATMIS na kitakuwa na jukumu la kuwakabili wanamgambo wa Al-Shabaab.Tumemuliza msikilizaji iwapo anaamini kikosi hiki kipya kitafanikiwa kuleta amani nchini Somalia

  • MADA HURU

    27/12/2024 Duración: 10min

    Tunakupa nafasi ya kuzungumzia tukio lolote lililotokea duniani wiki hii.  Tunakutakia sikukuu njema na maandalizi mema ya kuupokea mwaka wa 2025

página 1 de 2